Diamond, Babu Tale, Vanessa Mdee, Professor Jay wahofia usalama wa Roma Mkatoliki na wenzake waliotekwa usiku wa Jumatano

Rapper Roma Mkatoliki na vijana wengine walitekwa usiku wa Jumatano wakati walipokuwa studio ya Tongwe Records. Watu wasiojulikana walipotea na Roma na wenzake.

Mpaka sasa bado hakuna anayejua wamekamatwa na nani na kwa kosa gani, na pia bado haijafahamika wamepelekwa wapi. Lakini watu kwenye mitandao ya kijamii wanahusisha kitendo hiki na masuala ya siasa yanayoendelea nchini hivi sasa.

download latest music    
Roma Mkatoliki

Wasanii kadhaa wamekashifu kitendo hicho:

Professor Jay: ROMA MKATOLIKI AMEKAMATWA USIKU HUU… Nimestushwa sana kusikia kuwa kuna watu wamevamia studio za TONGWE RECORDS majira ya saa moja usiku na wamemchukua ROMA @roma2030 , MONI @moni_centrozone na kijana wa Kazi na pia wamechukua COMPUTER ya studio na Screen (Tv) na wameondoka navyo kusikojulikana.. Mpaka sasa hatujui wamewapeleka wapi!!

Diamond: Wakati mwingine natafakari sijui hata wapi tunaelekea… lla kwakuwa Mwenyezi Mungu ndio Mpangaji wa yote basi naamini hata hili litapita tu… Mwenyezi Mungu aipe nguvu familia ya @roma2030 na wanamziki wenzetu wote ambao hadi sasa haijajulikana walipo..

Vanessa Mdee: Wherever you are, God is Bigger than, Stronger than, Realer than all the other forces that be. Stay UP brother @roma2030 #VivaRoma #FreeRoma #FreeMoni roho inauma na nimetoka kumsikiliza mkeo redioni hajui hata ulipo sasa ndiyo nini ?????is this where we are at now? Ma studio yanavamiwa, watu wanakamatwa kama wanyama pori. Aaaarrrrgh

AY: Vyombo husika vifanye uchunguzi wa haraka tujue hali za wasanii wenzetu wako kwenye hali gani..@romamkatoliki Mungu yupo pamoja nanyi awaepushie lolote baya.. @tongwerecords @j_murder_tongwe

Babu Tale: Baba wa familia kupotea kama kuku na sisi wadau kuishi kupost tu hii sizani kama itatusaidia tuamke sote kwa pamoja saa sita mchana tukutane Tongwe Record tujue mstakabal wa mwenzetu @professorjaytz @efm_93.7 @cloudsfmtz #freeroma

 

About this writer:

Martin Oduor

Ultimate keyboard ninja dedicated to bringing you the juiciest stories on blogosphere