“Hamna bhana, mimi na Ema tunafanya tu kazi, mimi siko na Ema” Maua Sama

Kwa muda mrefu sasa, imekuwa inadaiwa Maua Sama amekuwa na uhusiano wa kimapenzi na producer wake Ema the Boy.

Maua Sama alizungumzia jambo hili na Soudy Brown na kukana hili jambo. Alieleza uhusiano wao ulikuwa wa kazi tu na hamna jambo lingine kati yao.

download latest music    

”Hamna bhana, mimi na Ema tunafanya tu kazi, mimi siko na Ema na watu wanatangaza tu kwani mimi ni mtu wa kwanza kutangaziwa vitu vya namna hiyo..?” Alinena.

Ema pia alimuunga mkono na kusema hivi;

“Sijui chochote kuhusu hizo habari. Mara nyingi tunakuwa tunarecord hamna kitu cha zaidi ya hapo. Wewe unajua mambo ya muziki yanavyokuwa, muda mwingine mnaweza kutoka asubuhi ukamrudisha anapokaa au usiku mkaenda wote kutafuta chakula lakini hamna chochote ni muziki tu.”

Na ndio hiyo sasa.

About this writer:

Irari Ngugi

Lover of life, lover of big boobs and certified celebrity squasher. Catch me if you can on facebook as Irari Ngugi