Harmorapa afungua roho na kusema anataka kumoa Wema Sepetu

Wema Sepetu anatajika kwa kupenda kuwa na uhusiano wa kimapenzi na mstaa; aliwai kuwa na uhusia na Ali Kiba, Diamond and Idris Sultan.

Kwa sasa Wema hana mshikaji yeyote na hii ndio sababu ya Harmorapa kujitokeza na kusema kwamba angependa kumoa Wema.

download latest music    
Harmorapa

Msanii huyu amefungua roho na kusema kama angekubaliwa na Wema basi atatangaza ndoa mara moja.

“Napenda kusema ukweli ulio jificha moyoni mwangu tangu siku nyingi kutokana na jinsi ninavyo sumbuliwa na hisia za kimapenzi kwa mrembo @WEMASEPETU,tangu naanza kumfaham wema sepetu na kumwona kweny tv akigombea umiss tz mwaka 2006 nilitokea kumpenda sana na kupata hisia za kumwoa endapo ntampata basi tu ndo vile nilikua sina uwezo wa kuonana nae wala kukutana nae kwa sababu ya position nilio kua nayo enzi hizo nauza pochi mwenge?nakumbuka kipind kile #WEMASEPETU wamemkata kweny uchaguz wa wabunge wa viti maalum niliumia sana,hadi skupatwa na usingiz nakumbuka niliamka saa 9 za usiku gheto na kuelekea mwenge kulangua mikoba kwa sababu ya kuiuza kipindi npo maeneo ya mwenge rafiki yangu alie kua na smart na alikua akifaham ni kiasigani namkubari #wemasepetunga alinipa taarifa kua #sepetunga anaingia dar kutokea dodoma baada ya jina lake kukatwa Ukwel nilisema lazima nikampokee na dhawadi nimpatie, bas nikaingia zangu kurangua mikoba nilibahatika kupata mkoba mmoja mzuri sana Akili ikanijia kua ule mkoba nmpe dhawad #kiumizaRohoYangu sikuuza nikauhifadh baadae nikafunga gori langu mapema nikaelekea kumpokea #kiumizaRohoYangu baada ya madam kufika niliangaika sana ili nimpatie ile dhawad ya mkoba bahati mbaya niligongwa na bodaboda kweny mguu wa kushoto na skufanyikiwa kumpa ila hadi leo ule mkoba nnao endapo siku nikipata fursa ya kukutana nae ntampatia huo mkoba.

“Ila nachukizwa sana na vijana walio uchezea moyo wa #sepetunga wakina #Mrblue, #diamond,#idrisa na wengineo nawachukia sana kwa kuufanya moyo wa @WEMASEPETU kama danadana na kuwalaum juu.

“Pia nawaonya wale wote mnao mlinganisha #Zarithebosslady na #WEMASEPETU mnakosea sana wema sepetu n mzuri mno kuliko #zarithebosslady sio kwamba #Mamatee n mbaya hapana mamatee ni mzuri ila hajamfikia #wemasepetu.

“Yote ya yote naombeni mumfikishie Taarifa hizi #WEMASEPETU Mwambieni nampenda sana endapo nikampata hato chukua hata wiki kwangu ntamvisha pete na kufunga ndoa nae juu na kumtunza kwa hali yoyote ile,” Harmorapa aliandika.

 

About this writer:

Martin Oduor

Ultimate keyboard ninja dedicated to bringing you the juiciest stories on blogosphere