Hussein Machozi: Muziki wangu umeshika Kenya kuliko Tanzania

Hussein Machozi amerejea nchini Tanzania kutoka Italy, msanii huyo aliwasili jijini Dar es salaam usiku wa Jumatano.

Hussein alikua amesafiri kuenda Italy katika shughuli zake za masomo na muziki. Muimbaji huyo amerudi nyumbani akiwa na video yake mpya iliyoandaliwa Italy.

download latest music    

Akiongea na Bongo5, Hussein alisema kuwa hakuhamia Kenya kama wengi wadhaniavyo – muimbaji huyo amekaa Kenya sana na kufanya watu wengu kufikiri kuwa alihamia huko kabisa.

Hussein alisema kilichompeleka Kenya ni wimbo, alieleza kuwa anapata riziki kubwa Kenya kuliko Tanzania kwasababu muziki yake umeshika sana huko.

“Kenya nlikwenda kama nlivyokwenda Italy, jabo Italy ntarudi tena sababu sijamaliza kitu ambacho nlikua nafanya. Kenya nlikua nimeenda tu kwasababu kwanza huko ni nchi jarani alafu tena pia muziki wangu Kenya ulikua umeshika, umeshika hadi leo. Kwa hivyo riziki ulikua unapatika kule kubwa kuliko Tanzania…kwani nkajikuta mara nyingi naenda Kenya narudi Tanzania…Mbaka watu wengine walikua wanasema nimehama lakini hapana,”alisema Hussein Machozi.

 

About this writer:

Martin Oduor

Ultimate keyboard ninja dedicated to bringing you the juiciest stories on blogosphere