Jifunze Kufanya Mambo Magumu Kuwa Rahisi

Watu wamekuwa wakikata tamaaa sana katika maisha tena hasa wanapokutana na vikwazo katika jambo wanalotaka kufanya, kitu cha kujua ni kwamba hakuna jambo linalokuwa zuri kabla halijakuumiza kichwa.Lakini kwanini uangaike na ukate tamaa katika maisha wakati ipo jinsi unaweza kuyafanya yaliyo magumu kuwa rahisi na ukafanikiwa.Hebu angalia njia hizi zinavyoweka kukufanya ufanikiwe na ukaacha kukata tamaa ya kufanikiwa kitu.

  • Ni rahisi sana  kufanikwa jambo lolote lile endapo  endapo jambo hilo utaweza kulifanya mara moja bila kusubiria au kuweka sababu zisizo na maana.
  • Ni rahisi kujifunza kitu kipya kila siku katika maisha endapo utaiandaa akili yako katika kujifunza , hii itakusaidi wewe kutoka kwenye kushindwa na kujaribu mbinu mpya ili kufanikiwa zaidi.
  • Ni rahisi kusogea kimaisha kutoa hapo ulipo endapo tu utaweka akili yako katika kutoka hapo ulipo na kupanda ngazi za juu zaidi.
  • Ni rahisi kuwa na watu watakao kutia moyo siku zote endapo na wewe utakuwa mstari wa mbele katika kuwatia moyo waliopo pembeni yako.
  • Ni rahisi kuweka akiba na kuanza kukuza utajiri ,endapo kuanzia leo utaamua kufanya utekelezaji wa hilo.Hii itakufanya kutatua hata yale majukumu yanayosemwa hayawezekani endapo wewe utaligawa ilo jukumu na kulifanyia kazi.
  • Ni rahisi kukuza kipato chako kama utaamua kujifunza kuweka akiba  kidogo kidogo.
  • Ni rahisi kuyafanya maisha yako  yakawa ya maana sana  ikiwa kila siku utachukua jukumu la  kufanya mabadiliko kidogo kidogo.

Maisha yako yanweza kuwa kama unayotaka yawe endapo utaifanya akili yako kubeba jukumu ya kuyaweka vile unataka yawe tena na kila kitu chako kikiwa tayari kufanikisha jukumu ilo.

download latest music    

Acha kufanya maisha yako yakawa magumu kwa sababu tu kuna mazingira uliyapitia ukahisi hayawezi kuabdilika kamwe.

Siku ozte weka kichwani kuwa ni kitu rahisi sana kufanya jambo jipya na kunza upya kwa jambo lolot ilimradi tu ujue pale ulipokosea mara ya mwisho ulipoanguka ni wapi.

Unapoamua kufanya mabadiliko katika maisha ustake kufanya kwa haraka, fanya vitu taratibu kwa uwezo wako bila kukata tamaa na uwe mtu wa kuinuka na kujirekebisha na kujifunza kila siku .

About this writer:

Expedicto Lilian

#Godseeker, I am what i ought to be and always i will be, but am not what i used to be.