Juma Nature afunguka baada ya Harmorapa kudai kuwa alikuwa anamdai baada ya collabo yao

Image: Juma Nature

Imemchukua Juma Nature wakati kuzungumza kuhusu maneno ambayo Harmorapa aliyosema hivi karibuni akiwa kwenye interview na kipindi cha E News cha EATV. Kulingana na ripoti zinazoenea kwenye mitandao jamii Harmorapa anadai kuwa Juma Nature anamdai pesa ya mavazi aliyovaa kwenye wimbo wake mpya ‘Kiboko Ya Mabishoo’.

Harmorapa
Harmorapa

Harmorapa alisikika akisema,

download latest music    

“Haipo sawa kwa wasanii wakubwa kutudai sisi ‘underground’ pesa ya kufanyia collabo wakati wanajua bado hata hatuanza kufaidika na muziki wenyewe.”

Akizungumza kwenye Kipindi cha E news Juma nature pia alikanusha madai haya akisema kuwa Harmorapa hana pesa za kumlipa ata angekuwa anamdai rapa huyo hawezi kumlipa.

“Nikisema nimemlipisha Harmorapa pesa kwa ajili ya kolabo nitakuwa nakosea. Mimi ni mtu mzima nilikubali kufanya wimbo na msanii yule kwa sababu ni mkali na anajua muziki pia na imani atafika mbali. Hawezi kunilipa mimi, ana hela gani?

About this writer:

Pauline Syombua

Content Developer IG: Kermbua