Mchumba wa Aunty Ezekiel aeleza mbona hawezi kuwa muimbaji wa Wasafi records

Image: Mose Iyobo na Aunty Ezekiel

Moses Iyobo ambaye ni dancer maarufu wa Diamond Platnumz amefunguka kwa nini hawezi kuwa muimbaji ataiwapo angepewa fursa hiyo.

Akiongea na gazeti maarufu la Dimba, Mose alisema kuwa hana mipango ya kuingia katika muziki na kuwa kwa hivi sasa lengo lake ni kuwa dancer ambayo ni kazi anayoifanya kwa hivi sasa.

download latest music    
Mose Iyobo na Aunty Ezekiel
Mose Iyobo na Aunty Ezekiel

Kiluingana na yeye, kuwa muimbaji inatakiwa mtu kuwa na kipaji ambacho yeye mwenyewe hana kwa hivyo si kitu ambacho anaweza kufanya na kufanikiwa. Alisema,

“Unajua kuimba kunahitaji akili nyingi ili ufanikiwe, sasa kwa upande wangu sitaweza ni bora nibaki huku huku ndio pananifaa zaidi,”

Ata hivyo Mose Iyobo alisema kuwa angependa kuwa mwalimu wa kuwafindisha vijana kuwa dancer kama yeye. Kuna watoto ambao wangependa kuwa dancers wakiwa wakubwa kwa hivyo ni heri yeye kuanzisha shule ambayo atawafundisha ili hapo mbeleni waweze kutambulika kama yeye.

About this writer:

Pauline Syombua

Content Developer IG: Kermbua