Muimbaji wa nyimbo za injili Flora Mbasha alipata mtoto nje ya ndoa yake

Mume wa zamani wa muimbaji wa nyimbo za injili Flora Mbasha amedhibitisha kuwa msanii huyo alipata mtoto nje ya ndo kabla hawajaachana.

Emmanuel Mbasha na Flora Mbasha kabla hawajaachana

Emmanuel Mbasha alisema hayo akiongea na EATV siku ya Jumatano. Ishu hiyo imeibuka baada ya mmoja kati ya watu waliouliza maswali kumtaka Mbasha kueleza kuhusu mtoto wa pili wa Flora kama ni wake ama la.

download latest music    

Hapo awali Flora alikiri suala hilo wakiwa katika harakati za kuachana kwa mujibu wa sheria mahakamani, aliambia koti kuwa alizaa mtoto mmoja tu na mume wake Emmanuel.

Mtoto wao wa kwanza anayeitwa Elizabeth ndiye Flora alimzaa na mumewe wa kitambo, mtoto wa pili alimpata nje ya ndoa.

“Yule mtoto siyo wangu, hata katika hati ya mashitaka ya kuachanishwa na mahakama, yeye mwenyewe Flora kwa mkono wake akiwa na wanasheria wake, aliandika kwamba kwa kipindi chote ambacho aliishi na mimi alibahatika kupata mtoto mmoja pekee ambaye ni Eliza, kwahiyo mpaka hapo unajua kabisa kwa hapa imeshakula kwangu, ni kitu ambacho knauma sana, lakini kila mtu na ujasiri wake” alisema Emmanuel Mbasha.

 

 

About this writer:

Martin Oduor

Ultimate keyboard ninja dedicated to bringing you the juiciest stories on blogosphere