“Nliamini kuwa sitakuwa na wewe” Mke wa Roma Mkatoliki aeleza hofu iliompata baada ya bwana wake kupotea

Wiki chache zilizopita Roma Mkatoliki alitekwa nyara na watu wasiojulikana alipokua kwenye studio. Msanii huyo aliachiliwa huru baada ya wasanii kulalamika.

Soma pia: Roma Mkatoliki aelezea yote yaliyomfanyakia baada ya kutekwa

download latest music    

Mke wa Roma Mkatoliki, Nancy, alisherekea siku ya kuzaliwa kwake Jumapili hii Aprili 23. Nancy aliongelea kupotea kwa mumewe.

Alisema kuwa alikata tamaa kumpata mume wake baada ya siku kadhaa kupita bila kuskia lolote kutoka kwa polisi ama watu waliomteka nyara mumewe.

Nancy na Roma Mkatoliki

“lifika wakati nilikata tamaa na kuamini kuwa sitakuwa na wewe katika sikukuu ya kumbukumbu yangu ya kuzaliwa ya mwaka huu!! Lakini Mungu Baba Wa Mbinguni akasema no. #MyBirthday2017,” aliandika Nancy kwenye Instagram.

 

About this writer:

Martin Oduor

Ultimate keyboard ninja dedicated to bringing you the juiciest stories on blogosphere