Rais Magufuli ampigia simu Mwana FA

Rais John Magufuli amedhibitisha kuwa yuko makini na mambo ya kimuziki, hivi karibuni alipiga simu kuzungumza na Diamond alipokua akihojiwa kwenye Clouds FM.

Magufuli alimpigia msanii mwingine simu tena – Mwana FA. Rapper huyo alipokea simu kutoka kwa kiongozi wa taifa kumpongeza.

download latest music    

Rais aliamua kumpigia simu Mwana FA kumwambia kuwa ni msikilizaji mzuri wa ngoma zake. Magufuli alisema anapenda sana ngoma yake ‘Dume Suruali’ alioimba na Vanessa Mdee.

“Nimefurahi kupokea simu ya Mheshimiwa Rais @MagufuliJP kunisalimia na kuniambia yeye ni mpenzi wa kazi zangu,haswa #DumeSuruali,” Mwana FA alisema kwenye Twitter.

Tazama wimbo wake ‘Dume Suruali’ hapo chini:

 

About this writer:

Martin Oduor

Ultimate keyboard ninja dedicated to bringing you the juiciest stories on blogosphere