Ray C amshukuru sana Naibu Waziri wa Afya – Hamisi Kigwangalla kwa kumtendea hili

Hamisi Kigwangalla, Naibu Waziri wa Afya na Mambo ya Wanawake, amewasihi Watanzania wote wampe Ray C support yao yote kuliko wakati wowote ule.

Kigwangalla alisema kila mtu hukosa na kila mtu anahitaji nafasi ya pili ile kuweza kurekebisha makosa waliofanya. Waziri huyo alisema Watanzania wanafaa wampe Ray C nafasi ya pili.

download latest music    
Hamisi Kigwangalla

“Na Mimi kama Naibu Waziri wa Mambo ya Wanawake, kama #BaloziWaWanawake na kama Daktari niseme nimefurahishwa na kuvutiwa sana na jitihada anazofanya huyu dada @rayctanzania, nimeguswa na wimbo wake wa #Unanimaliza, na nimeona nimuunge mkono kwa kuwaomba wadau wote ambao mmekuwa naye siku zote mfahamu kuwa sasa anahitaji support yetu zaidi kuliko wakati wowote ule. Tumuunge mkono kwa dhati. Mungu atatujaalia kheir kwenye maisha yetu pia. Hakuna aliyekamilika. Sote tuna vipindi vyetu vya kuanguka Na kwa hakika tunahitaji ‘a second chance’ kila siku za maisha yetu! Hakuna anayeweza kujisimamia mwenyewe, sote tunahitaji mtu mmoja wa kutushika mkono na kutunyanyua pindi tunapoanguka! Kila la kheir Ndg. Rehema Chalamila. With our support, even the sky is not the limit! Keep on moving, keep on believing!” Hamisi Kigwangalla aliandika kwa Instagram.

Ray C alifurahiswa sana na maneno aliyosema  Kigwangalla, alimshuruku kwa dhati.

“Heshima kwako Mheshimiwa,Nashukuru sana kwa maneno yako ya Faraja baba.Bless Your Soul Sir ????  @hamisi_kigwangalla ,” Ray C aliandika.

Ray C

 

About this writer:

Martin Oduor

Ultimate keyboard ninja dedicated to bringing you the juiciest stories on blogosphere