Ray C hatimaye ampa jibu msanii kutoka Kenya – Ringtone aliyetaka kumoa

Mwimbaji wa nyimbo za Injili kutoka Kenya – Ringtone alitoa pendekezo akitaka Rehema Chalamila maarufu kama Ray C afunge naye ndoa.

Hii ilikua mwaka jana na Ray C hata hakumpa jibu. Ringtone ni msanii maarufu sana Kenya, amewahi fanya collabo ya nguvu na Christina Shusho. Wimbo wao ‘Tenda Mema’ bado ni hit kubwa sana.

download latest music    

Ringtone pia anadai kuwa msanii wa nyimbo za Injili mwenye utajiri mkubwa nchini Kenya. Ako na magari za kifahari na nyumba kubwa jijini Nairobi.

Ray C sasa amempa Ringtone jibu baada ya muda huo wote; akiongea na Mzazi Willy Tuva kenye kipindi cha Mambo Mseto ya Radio Citizen, Ray C alisema hawezi kubali Ringtone amuoe.

Ray C na Ringtone
Ray C na Ringtone

Mrembo huyo alikiri kuskia pendekezo la Ringtone kwenye mitendao lakini hakutaka kuongelea jambo hilo kwasababu hana haja nalo.

“Nilisoma hizo taarifa Kwa mitandao, namjua tu kama msanii kwanza wa Gospel, kwa hiyo nilishangaa sana ila ni mtu mzuri sana napenda anavyoshirikiana na wasanii wa Gospel wa Tanzania, ila hio haipo Kwenye ratiba yangu though,” Ray C alisema.

Ray C aliambia Mzazi Willy Tuva kuwa anampenda rais wa Kenya Uhuru Kenyatta and anaomba kukutana naye atakapoenda Kenya hivi karibuni.

About this writer:

Martin Oduor

Ultimate keyboard ninja dedicated to bringing you the juiciest stories on blogosphere