Ray C: Kujiua kwangu lilikuwa ni wazo la mara kwa mara

Ray C amefunguka huhusu jinsi alivyotaka kujitoa uhai zaidi ya mara 10 kutokana na panda shuka za mkondo wa maisha.

Hit maker huyo wa ‘Unanimaliza’ alijiingiza katika utumiaji wa mihadarati miaka ya awali jambo ambalo lilisababisha afya yake kuzorota na ata kulemaza kazi yake ya kimuziki.

download latest music    

Akizungumza na Wikienda katika mahojiano maalum, Ray C alisema kuwa nia ya kujitoa uhai ilikuwa ikitokana na yeye kuamini kuwa hakua na njia nyingine ya kujinusuru.

“Kujiua kwangu lilikuwa ni wazo la mara kwa mara, inaweza ikawa hata zaidi ya mara kumi kutokana na kukata tamaa kabisa ya maisha huku nikijitazama nilivyokuwa msichana mwenye ndoto nyingi lakini nateketea nikijiona.

“Kuna wakati nilikata kabisa tamaa kuwa hakuna njia nyingine ya kunifanya nipumzike na tabu niliyokuwa nikipata zaidi ya kujitoa uhai ambao kwangu haukuwa na thamani na wala sikuwa ninajipenda tena hata kidogo,” alisema Ray C.

 

About this writer:

Martin Oduor

Ultimate keyboard ninja dedicated to bringing you the juiciest stories on blogosphere