Roma Mkatoliki aeleza kwanini muziki wake sio chanzo cha yeye kutekwa nyara

Rapa Roma Mkatoliki na wenzake walitekwa nyara wiki kadhaa zilizopita wakiwa kwenye studio. Kupotea kwa Roma kulizua utata, watu wengi waliamini kuwa muziki anaoufanya Roma ndo ulikua chanzo cha yeye kutekwa nyara.

Roma alisemekana kuwa aliukosoa serikali kupitia mistari zake kwa wimbo wake, watu wengi walihusisha tukio la kupotea kwake na muziki anaoufanya.

download latest music    

Lakini akizungumuza katika kipindi cha Clouds 360 cha Clouds TV, Roma alikana dhana hilo. Alisema muziki wake hauvunji sheria yoyote.

“Kwanza niweke sawa, naamini katika muziki ninaofanya na naamini sijafanya kitu kibaya, sivunji sheria na wala siongei maneno mabaya

“Naumia sana nikiona mtu anautafsiri vibaya muziki wangu. Mimi sifungamani na upande wowote, hata ukiniuliza kadi ya chama mimi sina kadi ya chama chochote. Kwa sababu nikichukua kadi ya chama chako utasema nimekuwa mwanafamilia wako wewe ni baba ukikosea nitakunyooshea vipi kidole?. Kwa hiyo napata sana ukakasi nikiona watu Roma wanamtafsiri tofauti, naumia sana,”alisema Roma.

About this writer:

Martin Oduor

Ultimate keyboard ninja dedicated to bringing you the juiciest stories on blogosphere