Rose Muhando atoweka nyumbani kwake mjini Dodoma

Mwimbaji maarufu wa nyimbo za injili Rose Muhando adaiwa kutoweka nyumbani kwake baada ya kutopea kwenye matumizi ya dawa ya kulevya.

Mwandani wa mwimbaji huyo aliwaambia wanahabari kwamba Muhando alikua akisakwa na uongozi wa Sober House ya Pederef ili waweze kumwokoa na matumiza ya mihadarati.

download latest music    

“Kuna kiongozi mmoja wa dini hapa Dodoma, ameamua kujitolea kumsaidia Rose baada ya kusikia hali yake ni mbaya. Ameamua kuwatafuta Pederef ili wamsake popote alipo na wakimpata wampeleke soba moja kwa moja na gharama zote yeye atazishughulikia,” Chanzo kilicho karibu na Muhando kilisema.

Mmliki wa Sober ya Pederef, Nuru Saleh, alidhibitisha madai hayo alipoulizwa na wanahabari. Saleh alisema kwamba alimtafuta Rose Muhando na kumrudisha katika soba yao iliyopo Dodoma na kuanza kumpatia tiba ya kuacha matumizi ya madawa ya kulevya.

“Ni kweli. Sisi ndiyo kazi yetu. Nimepewa hiyo kazi na kiongozi wa dini, naomba nisimtaje lakini tumeshaanza kumtafuta na tukimpata tu, tutampeleka kwenye soba yetu ya Dodoma,” Nuru alisema.

 

About this writer:

Martin Oduor

Ultimate keyboard ninja dedicated to bringing you the juiciest stories on blogosphere