Saida Karoli aeleza kilichompa nguvu mpya ya kurudi kwenye muziki baada ya kustaafu

Mwimbaji mkongwe Saida Karoli anayejulikana kwa hit yake ‘Maria ya Salome’ amerejea kwenye sanaa ya muziki baada ya kupotea kwa miaka kadhaa.

Akiongea kwenye kipindi cha XXL cha Clouds FM Ijumaa iliopita, Saida Karoli alisema kuwa kurejea kwake kwenye muziki ulifanikishwa na Diamond na Belle 9.

download latest music    

Anadai kuwa Belle 9 na Diamond walimpa nguvu mpya ya kurudi kwenye muziki baada ya kuachia nyimbo zao walizotumia baadhi ya vitu kutoka kwenye wimbo wake wa ‘Maria ya Salome’.

“Nilishatamani kuacha muziki na nilishawahi kuhamisha baadhi ya vitu vyangu kurudi kijijini na ndiyo kipindi hiko hiko Belle Nine na Diamond walitoa nyimbo ya Chambua kama karanga, wakanirudisha maana ilikuwa safari kabisa,” Saida Karoli alisema.

Diamond and Saida Karoli

 

About this writer:

Martin Oduor

Ultimate keyboard ninja dedicated to bringing you the juiciest stories on blogosphere