Shilole: Mimi namkubali zaidi Diamond Platnumz kuliko Ali Kiba

Shilole ameeleza sababu ya kumkubali Diamond Platnumz kuliko Ali Kiba – wawili hao (Ali Kiba na Diamond) ni maadui wakubwa kimuziki.

Nani kati Diamond na Ali Kiba ndo mfalme wa muziki Tanzania? Mjadala huu huzua utata kila mara unapoulizwa. Mashabiki wa Diamond watasema Simba ndo anaweza na wale wa Ali Kiba watasema yeye ndo bingwa.

download latest music    

Zuwena Muhamed alimaarufu kama Shilole amesema yeye ni Team Diamond Platnumz. Akiongea kwenye kipindi cha Kikaangoni live kinachofanyika kupitia ukurasa wa facebook wa EATV, Shilole alisema yeye anamkubali sana Diamond.

“Mimi namkubali zaidi Diamond Platnumz kuliko Alikiba, nampenda Diamond kutoka na mambo yake na vile alivyo, kwa hiyo kila mtu ana watu anaowakubali na kuwapenda” alisema Shilole.

About this writer:

Martin Oduor

Ultimate keyboard ninja dedicated to bringing you the juiciest stories on blogosphere