Snura Mushi aeleza kwa nini hatamani kabisa kuhusiana kimapenzi na mtu yeyote maarufu

Snura Mushi ni mama wa watoto wawili, alizaa mtoto wake wa pili Januari 2015. Msanii huyo hajawahi kuwa kwenye uhusiano uliodumu muda mrefu.

Ata hivyo Snura hataki kuhusiana kimapenzi na mtu yeyote maarufu, alisema kuwa amekuwa akifuatilia uhusiano wa kimapenzi wa mastaa wengi na kugundua kuwa huwa haudumu kutokana na mastaa kutokuwa waaminifu au mazingira ya kazi zao ambayo kwa wasanii wa kiume yanawafanya kuwa karibu na wanawake.

download latest music    

“Naomba niwe muwazi, kwa sasa sitamani kabisa kutoka kimapenzi na mtu maarufu au niseme tu staa kutokana na mimi kuwa mtu mwenye wivu sana, unajua mastaa wengi wa kiume huwa karibu sana na wanawake kwa mazingira ya kawaida ya kikazi, sasa mimi nikiona hivyo ninafahamu ninasalitiwa tu,” Snura aliambia Uwazi Showbiz.

 

About this writer:

Martin Oduor

Ultimate keyboard ninja dedicated to bringing you the juiciest stories on blogosphere