Staa wa nyimbo za Injili Upendo Nkone atuma ujumbe maalum kwa Rais John Magufuli

Mwimbaji Upendo Nkone ametuma ujumbe maalum kwa rais Magufuli akimwambia kwamba yuko tayari kuitumikia jamii kupitia nafasi ya ubunge.

Nkone ata hivyo amesema hataki kujiunga na siasa kwa ubunge wa kugombea jimboni ila kama mbunge mteuliwa na Rais wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania.

download latest music    

Akiongea kwenye kipindi cha Kikaangoni cha EATV, Upendo alisema kuwa yuko tayari kuitumikia jamii kupitia nafasi ya ubunge iwapo Magufuli atamteua.

Upendo Nkone

“Sina mpango wa kuwa mwanasiasa, kwahiyo hata ubunge wa kugombea siwezi, lakini kama Rais wangu Magufuli akilala akiota kwamba anipe ubunge viti maalum, kwakweli napokea…. Mh. Magufuli nimeambiwa nigombee ubunge, basi unikumbuke baba,” alisema Upendo Nkone.

Nkone alisisitiza kuwa Rais Magufuli anapaswa kumteua kwasababu kuwa yeye mchakato wa kupata ubunge wa kugombea ni mgumu na una mambo mengi ikiwa ni pamoja na gharama, jambo ambalo haliwezi.

 

About this writer:

Martin Oduor

Ultimate keyboard ninja dedicated to bringing you the juiciest stories on blogosphere