Rayvanny Ampigia Salute Alikiba

Mwanamuziki anaefanya vizuri katia anga za muziki Raymond maarufu kama Rayvanny kutoka kundi kubwa nchini WCB amefunguka na kusema kuwa kati ya wasanii wakali anaowakubali nchini ninpamoja na alikiba pamoja na kwamba msanii huyo ni mshindani mkubwa wa bosi wake Diamond Platinumz.

Akiongea na Global online tv, Rayvannya ameorodjesha wasanii wakubwa tanzania ambao anafurahi jinsi wanavyofanya kazi hasa kujituma na kupeperusha bendera ya taifa na kusema kuwa wasanii hao ni pamoja na Diamond platinumz, Alikiba pamoja na Vannesa mdee ambao wamekuwa kama nembo ya taifa.

Katika hali ya kawaida amshabiki wengi wamekuwa wakihisi kuwa wasanii wengine wanapaswa kumchukia Alikiba kwa sababu tu amekuwa mshindaniwa siku nyingi wa bosi wao lakini , wcb imefika sehemu wanaonekana kuona kuwa bifu za wasaniihazijengi na ndio maana kwa sasa wanaonekana kujitahidi kuepukana na maneno ya uchochezi kutoka kwa mashabiki.