Askofu Gwajima aachiliwa huru na Mahakama

Askofu Gwajima sasa hivi yuko huru baada ya Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kumuachia baada ya upande wa mashitaka ushadi kukosa ushahidi wa kutosha baada ya kupelekwa kotini na Askofu Mkuu wa Kanisa Katoliki jimbo Kuu la Dar es Salaam, Mwadhama Polycarp Kadinari Pengo.

Kulingana na malalamishi ya Askofu Mwadhama inasemekana kuwa Gwajima alitumia lugha chafu na kuharibu jina la Mwadhama. Hata hivyo kesi hii imetupiliwa mbali baada ya upande wa mashitaka kushindwa kuleta mashidi kwa muda wa miezi 14.

Hata hivyo wakili wa Serikali, Joseph Maugo aliomba mahakama kuhairisha kesi hiyo ili kuwapa muda tosha wa kupata mashahidi katika kesi badala ya kesi hiyo kufutwa.

Gwajima anasemekana kuwa aliluita Askofu Mwadhama Polycarp ; Ni mpuuzi mmoja mjinga mmoja asiyefaa mmoja anaitwa Askofu Pengo aliropoka sijui amekula nini mimi naitwa Gwajima namwita mpuuzi yule mjinga yule na kuonesha Pengo ni mtoto mpuuzi na mwenye akili ndogo na kwamba maneno hayo yangeweza kuleta uvunjifu wa amani

Haya ndiyo maneno Halima Mdee alimjibu Askofu Gwajima baada yake kumkashifu mitandaoni

Mbali na kuhubiri, Askofu Gwajima amekuwa akizungumzia mambo mengi yanayohusu Tanzania. Alianza na Diamond na leo aliongelea mbunge wa Kawe, Halima Mdee ambaye alihutumiwa kwa kutoa lugha chafu bungeni.

Hivi ndivo alivyomweleza:

“Kwenye bunge kulitokea mbadilishano wa maneno kwenye uchaguzi wa wabunge wa Afrika Mashariki, inaonekana kuna mahali Chadema hawakutendewa vizuri. Kwenye mabishano hayo mbunge wangu wa Kawe akamwambia spika ‘wewe ni fala.’ Halima hilo jambo si sawa, hilo jambo sio sawa hatuwezi kukemea wengine wewe tukakuacha hilo jambo sio sawa. Ni kweli uliudhika, ni kweli ulikasirika lakini namna ya kuonyesha hasira yako sio kumtukana mtu ambaye ni mtu wa muhimili, ili Tanzania iwe vizuri nenda kaombe msamaha yaishe,”alisema.

“Ni lazima mtu yeyote anayeongoza wananchi awe mfano kwa maneno, vitendo na kwakuwa na moyo wa kuzuia hasira yake. Uwe na uwezo wa kubeba mambo, ukishindwa kujizuia na kumtukana Spika, watoto wanaosikia wanadharau nchi.”

Aidha alisema mbunge huyo kuwa hata kama aliudhika ni afadhali angejiangusha chini na kupiga kelele kuonesha hasira yake na si kutukana. Aliendelea kwa kuongeza kuwa “Koma, acha, wewe ni mbunge mzuri na mimi ni rafiki yako nakuambia ukome kumuambia maneno mabaya Spika.”

Na Halima Mdee akamjibu hivi:

“Namuheshimu sana Mch.Gwajima,sitajibizana nae kwenye mitandao. Niweke rekodi sawa sijamtukana na wala sitarajii kumkosea heshima Spika. Hayo ya J2 namwachia yeye! Yangu na yaliyojiri Bungeni.. Najua jinsi ya kuyahandle. Yawezekana yalishamalizwa kabla ya Ibada yake LEO.”