Fid Q Aingilia Kati Sakata la Roma na BASATA.

Rapa Fareed Kubanda maarufu kama Fid Q ameamua kuchukua jukumu la kuanzisha mazungumzo na Baraza la Sanaa Tanzania baada ya kutolewa kwa adhabu kwa msanii mwenzake wa muziki Roma Mkatoliki na kumfungia kwa kipindi cha miezi sita kutokufanya kazi yoyote ya muziki.

Fid Q alikuwa ni mtu wa kwanza kuonyesha hisia zake za kuumia na hukumu hiyo huku akiamini kuwa miezi sita ni minhi sana kwa msanii roma kutokana na ukweli kwamba msanii huyo ana familia yenye mke na watoto wanaomtegemea kupitia kazi hiyo.

waswahili wanasema mambo ya kusadifu ni kutosheleza haja  ya chunguni , yale yaletayo faida  kama chakula n.k, tunaomba mturuhusu tuje tujadili hii sheria ya kifungo upya siu ya jumatatu ili kumuokoa baba anayetegemewa na familia kwa kupitia sanaa.

Kupitia ukurasa wa Twitter, Baraza la Sanaa pia lilimaua kumjibu Fid Q na kumtaka akaribie kwa ajili ya mazungumzo ya swala la msanii huyo.

milango iko wazi muda wote,Baraza limesukumwa kuundwa kwa umoja  wa wasanii na kujenga mfumo rasmi wa mawasiliano na majadiliano .bahati mbaya wasanii wengi bado wako nje ya mfumo huo.Limekuwa  likiitisha vikao vya mashauriano , lakini mahudhurio yamekuwa hafifu .Kupitia umoja uliopo karibuni.