Tigo Fiesta Kuunguruma Tena Jijini Dar Wiki Ijayo

Tamasha maarufu nchini Tigo Fiesta la mwaka 2018 linatarajiwa kufanyika rasmi jijini Dar Wiki ijayo ya Tarehe 22 katika viwanja vya Posta.

Fiesta tayari ilifanyika karibia mikoa 15 nchini Tanzania lakini ilipofika wakati wa kufanyika hapa Dar Es Salaam ambayo ndio ilikuwa inafunga msimu mpya wa Fiesta ilisitishwa kwa madai kwamba sehemu ambako ingeenda kufanyika ingeleta taharuki kutokana na kelele zitakazojitokeza mahala hapo.

Uongozi wa Clouds Media Group Kupitia ukurasa wao wa Instagram umetoa taarifa hii kuhusiana na tamasha hilo:

Tarehe 22 Desemba kwenye Viwanja vya Posta jijini Dar es Salaam, Machampion wote wa nchi wanakwenda kutoa shukrani moja kubwa na kushangalia mafanikio ya mwaka huu. Ni mara 2 ya tulichokimiss: stage ya viwango, sound kubwa kuliko, bata la kihistoria na list ndefu ya machampion. . #TigoFiesta2018, ” 

Nandy Atupwa Kando Kwenye Listi Ya Wasanii 29 Watakaoperfom Fiesta

Clouds Media Group limetangaza Listi ya majina 29 ya wasanii ambao wanatarajiwa kuperfom katika tamasha la Fiesta 2018 litakalofanyika siku ya Jumamosi katika Viwanja vya Leaders Club.

Kwenye orodha hiyo ndefu, wapo wasanii Kama Rostam, Weusi, Maua Sama, Wakazi, Ben Pol, Chege, Fid Q na wengineo, huku wasanii chipukizi nao wakipewa kipaumbele.

1. Weusi  2. Rostam 3. Fid Q 4. Wakazi 5. Rich Mavoco  6. The Mafik 7. Ben pol 8. Rosa Ree 9. Marioo 10. Barnaba  11. Billnass 12. Chege Chigunda 13. Dogo Janja 14. Msami 15. WhoZu  16. Mimi Mars  17. Lulu Diva  18. Zaiid  19.Mesen Selekta 20. Maua Sama 21. Tid 22. Qchief 23. Juma Nature 24.Jolie 25.Benson 26.Jay Melody 27.Mabantu
28.Brian Simba 29.Amber Lulu”.

Suala la kukosekana kwa Msanii Nandy ambaye yupo ndani ya THT limeshangaza watu wengi huku tetesi za chini ya kapeti zikidai kuwa huenda kitendo cha Nandy kuonekana akila bata na Diamond Platnumz Dubai kinaweza kuwa chanzo.

Baada ya tetesi nyingi kusambaa Baada ya jina la Nandy kukosekana Clouds wametoa kauli na kusema kuwa List nyingine ya kambi ya upinzani itatangazwa baadae

N.B kuna Listi ya kambi ya Upinzani bado.  Kama vipi Jumamosii hii tukutane Leaders Club. Kiingilio 10,000/- Ukinunua kwa Tigopesa master-pass QR, na shs 15,000 Kawaida!“.