Daimond Atoa Sabau ya Kuimba wimbo Uliokatazwa.

Msanii wa muziki Bongo Fleva, Diamond ameleza ni kwanini walitumbuiza wimbo wa ‘Mwanza’ ambao tayari ulikuwa umefungiwa.

Muimbaji huyo kutoka WCB akizungumza na Wasafi TV amesema kuwa walilazimika kufanya hivyo mkoani Mwanza wakati wa tamasha la Wasafi Festival kutokana na uhitaji kuwa mkubwa.

“Unajua mimi ndio nilikuwa naomba sana, halafu Mwanza walikuwa wanaomba huo wimbo sana, hadi watu anatingisha jukwaa, sasa tukaangalia ushafika muda kama saa tisa watoto hamna, watu wamelala ikabidi tuamshe ili mashabiki wasione tunawaletea pozi,” amesema Diamond.

Wimbo Mwanza maarufu kama Nyegezi ambao ni wa Rayvanny akimshirikisha Diamond,umefungiwa na Baraza la Sanaa Taifa (BASATA) kutokana na kukiuka maadili.

Diamond , Majjizo Wamsusa Hamisa Mobeto

Mwanadada Hamisa Mobeto siku ya Novemba 10 amesherekea siku yake ya kuzaliwa huku salamu nyingi zikitoka kwa watu mbalimbali kila mmoja kimtakia kheri na baraka katika siku yake hiyo.

Hamisa mwenyewe amekuwa akisherekea siku yake ya kuzaliwa kwa kutoa zawadi kwa watoto wenye uhitaji kuitia foundation yake ya Mobeto foundation, hata gvyo kama ilivyokuwa haikutegemewa ni kwamba wanaume ambao waliwahi kuwa katika mahusiano na mwanadda huyo wameshindwa kumtakia kheri katika siku yake hiyo.

Diamond pamoja na majizo ambao walibahatika kupata watoto na mwanadada huyo wameweka attention kubwa ka mashabiki wao kwa sababu ni moja ya walitegemewa kufanya hivyo kwa sababu ya mahusiano ya  kizazi  baina yao.

kwa mwanaume mya ambae inasemekana kuwa ni mpenzi wa hamisa kwa sasa kutoka marekani ameweza kumu-wish mwanadada huyo kheri ya siku yake ya kuzaliwa.