Baada ya Kushambuliwa na mashabiki, Diamond Afika Msibani

Baada ya msanii Daimond kushambuliwa kwa muda mrefu na hata wasanii wenzake kutuma salamu kumuomba kufika katika msiba wa mkurugenzi wa Clouds media Group bwana Ruge mutahaba , hatimaye msanii huyo alifanikiwa kufika msibani.

Ingawa hakuruhuiswa kuingia mpaka ndani ambapo walikuwa wamekaa wasanii wengine na wageni wa VIP kutokana na kuchelewa kwake na umati wa watu wengi kumfuata kwa nyuma.

Hata hivyo msanii huyo alifika msibani akiwa na  walinzi wengi na kufuatwa  na watu wengi  akiwa ameongozana na familia yake ambayo ni dada yake ESMA na mama yake Mama Dangote.

Hata hivyo msanii huyo hakukaa muda mrefu msibani hapo aliamua kuondoka na group lake la wasanii aliokuja nao katika msiba huo.