Emmanuel Mbasha asema kuwa Flora hakumkimbia kutokana na ukosefu wa pesa

Muimbaji wa nyimbo za injili Tanzania, Emmanuel Mbasha amefunguka kwa mara ya kwanza baada ya mama ya watoto wake Flora kufunga ndoa na mwanaume mwingine.

 

Emmanuel Mbasha ambaye ni mmoja wa waimbamji maarufu Afrika mashariki ameweka wazi kuwa hana tatizo lolote na mwanaume aliyemuoa Flora. Hata hivyo alitaka watu kujua kuwa Flora hakumtoroka kwa sababu hakuwa na pesa lakini ni kwa sababu ya maisha mbayo yeye mwenyewe alitaka.

“Jamaa ambaye amemuoa Flora sina shida naye, anaweza kuwa mtu ambaye ananihofia kuwa nikikutana naye naweza kumdunda.Ila huyo jamaa mimi simchukii na wala simjui. Hajawahi kuniingilia kwenye issue yangu yoyote ya mapenzi ila mimi namchukia jamaa ambaye aliniingilia kwenye ndoa yangu ndiye mbaya wangu, na Watanzania wote wanamjua,”alisema Mbasha.

Hata hivyo anawatakia kila la heri kwenye Ndoa yao.