Hawa Atoa Shukrani Zake Kwa Diamond na WCB Baada Ya Kumaliza Matibabu

Msanii wa Bongo fleva Hawa Said maarufu kama Hawa ntarejea wa Diamond amevunja ukimya Mara Baada ya kumaliza matibabu nchini India na kumshukuru Diamond na WCB.

Msanii Diamond Platnumz na timu nzima ya WCB ndio ilisimamia matibabu yote ya Hawa mpaka anapiga kabisa Baada ya kuugua mpaka kutaka kufa miezi michache iliyopita.

Mrembo huyo amemshukuru Mungu pamoja na Watanzania kwa dua zao kwani mpaka sasa anaendelea vizuri na uvimbe wa tumbo umeondoka kwa asilimia kubwa.

Kupitia ukurasa wake wa Instagram, Babu Tale ameweka wazi salamu kutoka kwa Hawa:

https://www.instagram.com/p/BqM4FSDlEiw/?utm_source=ig_share_sheet&igshid=1ex61xjcr1qbp

Awali msanii huyo wa kike aliripotiwa kuumwa ugonjwa wa ini lakini alipofanyiwa vipimo nchini India walimkuta na ugonjwa wa moyo.

Babu Tale Aweka Wazi Hali Ya Kiafya Ya Hawa Kwa Sasa

Meneja wa staa wa Bongo fleva nchini Diamond Platnumz, Babu Tale ameweka wazi kuwa Mwanadada Hawa Saidi ambaye alikuwa anatibiwa nchini India anaendelea vizuri.

Hawa alikuwa na tatizo la ini ila ni moyo ndio uliokua unapelekea mgonjwa kujaa maji mwilini na Babu Tale ndio alipewa jukumu la kusimamia matibabu yake nchini India kwa kuwa gharama zote za matibabu alizitoa Diamond Platnumz.

Hawa alikuwa na tatizo la ini ila ni moyo ndio uliokua unapelekea mgonjwa kujaa maji mwilini na Babu Tale ndio alipewa jukumu la kusimamia matibabu yake nchini India kwa kuwa gharama zote za matibabu alizitoa Diamond Platnumz.

Kupitia ukurasa wake wa Instagram, Babu Tale amesema wazi kabisa kwa sasa Hali ya Hawa inaridhisha kabisa tofauti na siku chache zilizopita kabla ya kupata matibabu:

Diamond aliweka wazi kuwa ametumia zaidi ya milioni 490 kumtibia Hawa ambaye miezi michache iliyopita alikuwa hoi kitandani nchini Tanzania.