Jay Z atajikuna kichwa akiskia alichosema Joh Makini

Joh Makini amesema yuko katika kiwango ambayo hakuna rapa mwingine nchini Tanzania ambaye mashabiki wanaweza mfananisha na Jay Z.

Alitoa maoni haya baada mashabiki zake kumfananisha na msanii huyo wa Marekani ambaye ako na ushawishi mkubwa duniani mzima.

Jay Z

Joh anasema ufananisho wake na Jay Z ni dhibitisho tosha kuwa muziki wake upo katika kiwango kingine ambacho wasanii wengine bado hawajafika.

“Jay Z ni ‘role model’ wangu…mimi naimba maisha ya sinoni daraja mbili na Tanzania na Jay Z anaimba maisha ya Brooklyn na Marekani, nafikiri nipo katika ‘level’ ambayo hawaoni mtu mwingine wa kunifananisha naye…Kwahiyo mimi naona poa kwa sababu kama unanifananisha na Jay z ‘yeah i like it’ kuliko ungenifananisha na mtu mwingine,”Joh Makini alisema.