Jokate asimulia jambo ambalo lilimfanya kulia sana hivi karibuni

Jokate ambaye anajulikana sana Afrika Mashariki kwa filamu zake za uigizaji amefunguka kwa mara ya kwanza kueleza kitu ambacho kilimfanya kulia hivi karibuni.

Akizungumza kwenye interview Jokate alisema kuwa anavunjika roho kumuona mamake mzazi akimshughulikia baba yake ambaye kwa hivi sasa ni mgonjwa. Mrembo huyu aliendelea kwa kusema kuwa mama yake anatumia nguvu zake zote kuhakikisha kuwa baba yake amepona.

Aliendelea kwa kusema kuwa jambo hili linamuumiza sana kumuona mamake akijishughulisha sana kumsaidia baba yao ambaye a naumwa. Jokate alisema…

Kusema kweli hivi karibuni nimelia sana, baba yangu anaumwa sasa mama yangu anatumia nguvu kubwa kumuudumia kwa sababu baba anahitaji uangalizi wa karibu sana,”

Hata hivyo aliongeza kusema kuwa anatamami kuwa na familia yake lakini kwa hivi sasa bado hajampata.