Madee anyenyekea baada ya Wolper kumchambua mtandaoni

Msanii wa bongo Madee amejieleza baada ya ishu kubwa kutokea kati yake na muigizaji wa filamu za bongo Wolper.

Hii ilitokea baada ya Madee kutumia picha ya katuni inayofanana na Wolper kwenye wimbo wake mpya aliomshirikisha Tekno.

Kulingana na Wolper, Madee hakumuomba ruhusa ya kutumia picha yake na ndioi ikasababisha ishu hii.

Hata hivyo, akizungumza na Showbiz, Madee alisema, kuwa Tekno alitaka kutumia msichana mweupe na mwenye sifa tofautitofauti na ndipo Madee aliwaza na kumtumia Wolper. Lakini aliomba msamaha kwa makosa yake alisema;

“Nilikosea kumtumia Wolper kwa sababu kwanza sikumuomba. Wolper ni mshkaji nitawasiliana naye ili tuweze kulimaliza,”

 

 

Madee atisha baada ya kuonyesha gari ‘yake’ mpya

Msanii wa Bongo Madee ni mmoja wa watu ambao wanapenda kuonyesha vitu vyao vya thamana mitandaoni. Kama sio saa ni viatu ama kitu kingine.

Lakini hivi karibuni aliwaacha mashabiki wake kama wameduwaa baada ya kuonyesha gari ambalo lina jina lake kwenye number plate.

Hata hivyo Madee hakudhibitisha kuwa gari hilo ni lake lakini aliandika kusema, “Gangster paradise!!! #WinoMweusi,” huku akiwapa mashabiki wake nafasi ya kubashiri ikiwa amenunua gari.

Kama kawaida wengi walimpongeza na wengine wakimsomea kwa kuwaringia na gari ambalo wanajua sio lake. Madee hata hivyo hakuwajibu kwani yeye anaishi maisha ya super star.

Tazama gari hilo hapa.