Man Walter Achochea Bifu La Diamond na Ali Kiba Liendelee

Mtayarishaji wa muziki wa Bongo fleva Man Walter ameibuka na kusema kuwa anatamani Bifu kati ya wasanii wa Bongo fleva Diamond Platnumz na Ali Kiba lisiishe kabisa.

Man Walter amedai kuwa kuisha kwa bifu kati ya Ali Kiba na Diamond ni sawa na kuua timu za Simba na Yanga na hivyo kusababisha Kulia kaisa upinzani.

Kwenye mahojiano aliyofanya na Gazeti la Mwananchi, Man Walter ambaye ameshafanya kazi na wasanii hao wote wawili katika nyakati tofauti amesema Bifu hilo ndio Linapeleekea muziki kuwa mtamu.

Yaani Hawa wasanii wakipatana ni sawa na kutokuwepo kwa simba na Yanga, hivyo waacheni waendelee hivyo hivyo kwani ndio burudani yenye we”.

Pia Man Walter amefika mbali zaidi na kusema anahisi kabisa kama Bifu hilo litaisha kwa njia moja au nyingine basi ni wazi kabisa muziki wa Bongo fleva utadorora kabisa.