Baraka The Prince Amuangukia Mange Kimambi.

Mwanamuziki Baraka The Prince amemuangukia Mange Kimambi na kumuomba msamaha baada ya mwanadada huyo kutoa taarif za siri ambazo hazijawahi kusikika mahali popote kuhusu mwanamuziki huyo kuwa na mahusiano na mwanadada kutoka bongo movies.

Mange Kimambi ambae amkeuwa akitoa siri na kukosoa wasanii wengi kila kukicha siku ya jana alimuamkia Wema sepetu baada ya wema kuonekana kulivalia njuga swala la Hamisa kutaka kuiloga familia ya kina diamond kama voice notes iliyovuja ilivyokuwa ikisema.

Hata hivyo baada ya Mange kuamua kutoa siri za Wema moja kati ya vitu alivyoongea ilikuwa ni kwamba mwanadada Wema alishawahi kuwa na mahusiano ya kimapenzi na BARAKA lakini haikuwahi kufahamiaka hapo kabla.

Baraka The Prince kupitia ukurasa wake aliamua kuandika barua ya wazi kwa Mange huku akimuomba asimuharibie muziki wake kwa kutangaza habari kama hizo ambazo hazina ukweli ndani yake.

Baraka anamuomba mange kuangalia upy vyanzo vyake huku akimuelezea kuwa amekuwa akiangaika sana kutengeneza jina lake na brand yake hivyo akimchafua kwa sasa anakuwa kama anamuharibia sana.

Baraka aliwaomba mashabiki wake msamha akwa kilichoandikwa katika page ya mwanadada huyo huku akiaknusha kuwa kuliwahi kuwa na ukaribu wa kiampenzi kati yake na Wema sepetu na kusema kuwa amekuwa akimheshimu sana Wema .