Mh Lusinde awagomea BASATA kuhusu Wimbo wa Mwanza.

Moja ya wabunge katika bunge la jamhuri ya muungano wa tanzania mh lusinde kutoka mtera amefunguka na kuwataka baraza la sanaa kuacha kufanya kazi za ubabaishaji kwa kutaka kufanya kazi na kutoa hukumu za wasanii kulingana na klosa husika na sio kwa kuwakomoa wasanii.

Lusinde anasema kuwa basata wamekuwa wakifanya wasanii waishi kwa uoga wakati wana vipaji vya kuwafikisha mbali, Lusinde amesema hayo ikiwa ni siku cahche tangu BASATA walipotoa msamaha wa wasanii hao kuendelea kufaya show zao za nje ambazo zilsainiwa nje ya adhabu waliopewa kwa muda usiojulikana kutokana na kukaidi maagizo ya baraza hilo.

Wasanii hawa wawili kutoka WCB, Diamond na rayvanny wamepewa adhabu kwa muda usiojulikana kutokana nakuaidi agizo la kuacha kuimba wimbo huo jukwaani lakini wasanii hao waliimba wimbo huo , hivyo kuwafanya wapewe adhabu.

Mh lusinde anasema kuwa kama wimbo huo kuimbwa ni makosa basi hakuna haja ya kuwa na kata yenye jina hilo kwa sababu hata watu waapoitamka  basi wanakuwa wanatamka matuzi hivyo waachane nayo tu na kubadili jina hilo.

Hata hivyo mh huyo ametaja serikali kuingilia kati swala hilo kabla halijaonekana kuwa na mtazamo tofauti na wa wasanii wengine pia.