Gigy Money na Mo J Wazidi Kurushana Roho na Wapenzi Wapya

Video vixen na msanii wa Bongo fleva Gift Stanford maarufu kama Gigy Money na Baba Watoto Wake Mtangazaji wa Choice Fm Mo J wameendelea kurushana roho huku kila mmoja akimuanika Mpenzi Wake.

Gigy Money na Ex Wake Mo J wamelala Mtoto mmoj mwenye umri wa miezi Sita sasa lakini wamekuwa na tabia ya kuachana na kirudiana tangu Mtoto wao alivyozaliwa lakini hivi karibuni Gigy aliweka wazi kuwa wawili ho hawako pamoja tena.

Baada ya kuachana Gigy Money alimuanika wazi Mpenzi Wake ambaye yuko naye kwa sasa na kumtaja Kama Montana ambaye ni Mmarekani ambaye anaishi nchini Kenya.

Baada ya Gigy Money kuonekana akiwa anajiachia na jamaa huyo ingawa mara kwa Mara amekuwa akimsaliti na kurudi tena kwa Mo J hatimaye Mo J naye amechoka na kumuweka wazi Mpenzi Wake mpya.

Kupitia ukurasa wake wa Instagram, Mo J aemuanika mrembo huyo na kuambatanisha na kiemoji cha pete “? Soon Inshallah ??❤️” kumaanisha ameshibana na mrembo huyo na ndoa inaweza kutokea siku yoyote.