Mke wa Rommy Afunguka Mazito Baada Ya Mumewe Kumtongoza Naj

Wiki iliyopita Rommy Jones alizua gumzo baada ya meseji zake alizomtumia msanii Naj kwa ajili ya kumtongoza kuvuja kwenye mitandao ya kijamii.

Jambo hilo lilizua mambo mengi kwa sababu Rommy ametoka kuoa miezi michache iliyopita kwaiyo kitendo cha yeye kumtaka mwanamke mwingine kilishangaza wengi.

Lakini tangu siku ya Ijumaa mke wa Rommy Jones anayejulikana kama Kay Jord aliweka wazi kuwa hana mpango wa kuachana na mume wake kwa sababu ya michepuko.

Kwenye mahojiano aliyofanya na Ijumaa Wikienda mke wa Rommy amefunguka na kudai meseji hizo zilizodaiwa kwamba mumewe alikuwa akimtongoza Najma, haziendani na ukweli kwani asilimia kubwa zilionekana ulikuwa ni utani:

Nimesikia na watu wamesema mengi kuwa mimi nimeondoka nyumbani, kisa hizo meseji, jambo ambalo siyo kweli kabisa.
Hakuna ukweli kwenye jambo hilo ndiyo maana niliamua kukaa kimya”.

Kwa upande wake, Rommy alilieleza Ijumaa Wikienda kuwa, yeye ni mfanyabiashara na Najma wanafahamiana vizuri.
Alisema kuwa, kuhusiana na hizo meseji anazodai kumtongoza Naj ilikuwa ni utani wa kawaida tu.