Quick Rocka Afungukia Mahusiano na Kim Nana

Msanii wa muziki wa Bongo fleva  nchini Aboot Rocka maarufu kama Quick Rocka amefunguka kuhusu  mahusiano na mrembo ambaye ni video queen Lilian Kessy maarufu kama Kim Nana.

Kim Nana alijizolea umaarufu miezi michache iliyopita Baada ya kusemekana kuwa kwenye mahusiano ya kimapenzi na staa wa Bongo fleva nchini Diamond Platnumz.

Quick Rocka ameibuka na kukana kuwa kwenye mahusiano na mrembo huyo na kusisitiza kuwa mahusiano pekee aliyokuwa naye ni urafiki wa kawaida sana.

Kwenye mahojiano aliyofanya na Global Publishers, Quick Rocka amefunguka haya:

Ni kweli namfahamu Kim Nana kama mtu niliyekuwa nafanya naye kazi tu lakini hakuna mambo ya mapenzi kabisa.”

Tetesi za Kim Nana kutoka na Quick Rocka zilianza baada ya msanii huyo kuonekana anamposti mrembo huyo mara kwa Mara kupitia ukurasa wake wa Instagram.

Mwanamuziki Quick Rocka Ampigia Saluti Diamond Platnumz

Mwanamuziki wa Bongo fleva Quick Rocka ameibuka na kumpigia saluti Diamond na kudai kuwa rekodi yake aliyoiweka ni nguma kuivunja.

Diamond alivunja rekodi hiyo baada ya wimbo wake wa Hallelujah aliyomshirikisha Morgan Heritage kufikisha jumla ya views milioni moja ndani ya masaa kumi na tano na kufikisha milioni mbili ndani ya siku moja.

Kwa kupitia ukurasa wake wa Instagram mwanamuziki Quick Racka alituma video akimpa hongera Mwanamuziki mwenzake Diamond Platnumz na kumpongeza pia kwa video kali aliyofanya na pia kumsifia mwanamuziki Morgan Heritage aliyemshirikisha.

“Hatari mzee big shout out to Diamond Hallelujah is a dope song meen Morgan Heritage ameua we mwenyewe umeua you know what am saying so i appreciate good work brother and the video its a movie so big shout out to you one million views in fifteen hours man thats a record man ujue labda atokee mwingine avunje rekodi in twelve hours lakini rekodi hiyo ngumu sana kuvunjwa salute brother dope tune”.

Diamond alivunja rekodi iliyowekwa na Ali Kiba kupitia wimbo wake wa seduce me wiki chache zilizopita na pia  na pia Quick Rocka alimpongeza Ali Kiba kwa mafanikio yake.

Wewe umeupokeaje wimbo huo mpya wa Diamond  Je unahisi atatokea mwanamuziki wa kuvunja rekodi ya Diamond?

Tafadhali toa maoni yako.