Ujumbe aliyotoa Ray C kwa Chid Benzi kuhusu utumiaji wa dawa za kulevya

Rapa Chid Benzi ni miongoni mwa wasanii ambao walioathirika na matumizi ya dawa za kulevya. Afya yake Benzi ilikua ya kuogofya kabla ya menaja wake Diamond- Babu Tale kumpeleka Sober House kule Bagamoyo.

Chid Benzi akiwa amekonda alipoathiriwa na matumizi ya dawa za kulevya

Ray C, ambaye pia aliathirika na dawa za kulevya, amemuombea Chid Benzi kwa Mungu ili aweze kutoka rasmi kwenye mtihani wa dawa za kulevya.

download latest music    

Mrembo huyo alimpa moyo Chid Benzi kwa ujumbe aliyotoa, alisema kuwa anaamini rapa huyo ataweza kushinda vita dhidi ya matumizi ya dawa za kulevya.

Ray C alisema anataka Benzi atoka rasmi kwenye mtihani wa dawa za kulevya kwasababu anataka kutoa wimba nyingine na yeye.  Ray C and Chid benzi walishawahi kutoa wimbo pamoja – ‘Nihurumie’.

Ray C Alimsifu Benzi na kusema rapa huyo yupo miongoni mwa marapa wakali zaidi Tanzania. Alisema pengo aliyowacha Benzi linaonekana.

“Chid benzi ni bonge la msanii na kwa upande wa Hip hop nadhani ni ‘one of the best artist’ na kwa sasa hayupo pengo lake linaonekana. Nampenda sana Chid Benzi  na ninamuombea sana kwa Mungu aweze kutoka katika janga hilo la madawa na akirudi natamani kufanya nae kazi nyingine. Aweke nia naamini atatoka.

“Binadamu wote lazima wapitie mitihani lakini tatizo mitihani hiyo lazima itakuwa inatofautiana. Haifurahishi kabisa kumuona mtu anateseka na matumizi ya dawa .Kama binadamu lazima uwe na nafasi ya kujifikiria kwa sababu hakuna mtu anayeweza kubebea ugonjwa au matatizo. Naamini Mungu aliyenisaidia mimi nikatoka kule atawasaidia wote siyo Chidi tuu bali wote wenye nia ya kuachana na yale mateso,” alisema Ray C.

Chid Benzi

 

About this writer:

Martin Oduor

Ultimate keyboard ninja dedicated to bringing you the juiciest stories on blogosphere