“Uoga ni uzembe” Babu Tale amtaje anayemlaumu kwa kupotea kwa Roma Mkatoliki

Msanii Roma Mkatoliki na wenzake wamepotea bila ya yeyote kujua nani aliwateke, wamepelekwa wapi na nia yao ni ipi.

Wasanii wengi wamehofia usalama wa Roma na wenzake kwasababu hata polisi hawajui nani aliwateka. Watu wengi kwenye mitandao ya kijamii wanahusisha kitendo hiki na masuala ya siasa yanayoendelea nchini hivi sasa.

download latest music    
Roma Mkatoliki

Babu Tale, meneja wa Diamond, ameweka wazi kuwa mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam Paul Makonda ndiye anafaa kulaumiwa kwa kupotea kwa Roma.

Babu Tale amemtaka Makonda awaeleze Watanzania kule Roma alipo, anasema kuwa yeye ndiye kiongozi wa kamati ya usalama Dar es Salaam kwahivyo anafaa ajue Roma alipo.

Paul Makonda

Uoga ni uzembe me nazani mwenye jukumu la kujua Roma yupo wapi ni Mkuu wa koa sababu yeye ndio kiongozi wa kamati ya usalama ya mkoa sasa ikiwa tumezunguka vituo vyote vya polisi na mwenzetu atumuoni nani wa kumfuata kumwambia tunamtaka mwenzetu kama sio @paulmakonda me naanza hili bila uoga mkuu wa mkoa naomba utusaidie kutuambia mnzetu @roma2030 alipo. Tukutane Tongwe mida hii me nipo kwa foleni wakuu #uogauzembe#freeroma,” Babu Tale aliandika kwa Instagram.

 

About this writer:

Martin Oduor

Ultimate keyboard ninja dedicated to bringing you the juiciest stories on blogosphere