“Usinigeuze maji kesho, mana nakujua mzee wa single touch ukimuamulia mtu” Diamond amkejeli Askofu Gwajima

Beef kati ya Diamond na Askofu Gwajima ilianza baada ya askofu huyo kudai kuwa Diamond ni mshirika wa dini la kishetani la Freemasonry.

Askofu huyo alisema kuwa Diamond anamuimba kwa nia mbaya, aliapa kuwa angegeuza staa huyo kuwa maji lakini alibadilisha nia yake baada ya Diamond kumwomba msamaha.

download latest music    

“Yala! Yala! Jamani Mwenzenu nimeyatimba?….. lakini mi nafkiri watu wanatakiwa waiskilize hii nyimbo kwa umakini sana tena sana na wataelewa nini ilikuwa maana yangu haswa… Hususani kama kipengele nilichomtaja mzee wangu @Bishopgwajima nilisema: “mara nasikia vya aibu Konda na Gwajima eti ugomvi umekolea….ila kuchunguza kwa karibu ni kuna binti mmoja tu ndio kwa mitandao anachochea…

“Point yangu ni kwamba licha ya kweli kuna yaliyojiri nyuma, lakini kwa busara zao ninazoamini wamejaaliwa na Mwenyez Mungu muda si mref wangekaa chini na kumaliza…nawote kufurahi kwa pamoja, lakini kwakuwa kuna dada mwingine alikua anachochea hawa ndugu zetu wazidi kufarakana…ikapelekea hadi kufikia hapa…asa hapo kosa langu mie liko wapi??

“Chonde chonde mzee wangu @Bishopgwajima usinigeuze maji kesho ?, mana nakujua mzee wa single touch ukimuamulia mtu……. naweza jumapili ya kesho nikaiona chungu Mwaka mzima???” Diamond aliandika kwa Instagram.

Askofu huyo alimwonya Diamond tena alipokuwa akihubiria maumini wake Jumapili iliyopita, alisema kuwa Diamond akirudia kosa lake hatamsamea tena. Tazama video hio hapo chini:

 

About this writer:

Martin Oduor

Ultimate keyboard ninja dedicated to bringing you the juiciest stories on blogosphere