Haya ndiyo maneno Halima Mdee alimjibu Askofu Gwajima baada yake kumkashifu mitandaoni

Mbali na kuhubiri, Askofu Gwajima amekuwa akizungumzia mambo mengi yanayohusu Tanzania. Alianza na Diamond na leo aliongelea mbunge wa Kawe, Halima Mdee ambaye alihutumiwa kwa kutoa lugha chafu bungeni.

Hivi ndivo alivyomweleza:

download latest music    

“Kwenye bunge kulitokea mbadilishano wa maneno kwenye uchaguzi wa wabunge wa Afrika Mashariki, inaonekana kuna mahali Chadema hawakutendewa vizuri. Kwenye mabishano hayo mbunge wangu wa Kawe akamwambia spika ‘wewe ni fala.’ Halima hilo jambo si sawa, hilo jambo sio sawa hatuwezi kukemea wengine wewe tukakuacha hilo jambo sio sawa. Ni kweli uliudhika, ni kweli ulikasirika lakini namna ya kuonyesha hasira yako sio kumtukana mtu ambaye ni mtu wa muhimili, ili Tanzania iwe vizuri nenda kaombe msamaha yaishe,”alisema.

“Ni lazima mtu yeyote anayeongoza wananchi awe mfano kwa maneno, vitendo na kwakuwa na moyo wa kuzuia hasira yake. Uwe na uwezo wa kubeba mambo, ukishindwa kujizuia na kumtukana Spika, watoto wanaosikia wanadharau nchi.”

Aidha alisema mbunge huyo kuwa hata kama aliudhika ni afadhali angejiangusha chini na kupiga kelele kuonesha hasira yake na si kutukana. Aliendelea kwa kuongeza kuwa “Koma, acha, wewe ni mbunge mzuri na mimi ni rafiki yako nakuambia ukome kumuambia maneno mabaya Spika.”

Na Halima Mdee akamjibu hivi:

“Namuheshimu sana Mch.Gwajima,sitajibizana nae kwenye mitandao. Niweke rekodi sawa sijamtukana na wala sitarajii kumkosea heshima Spika. Hayo ya J2 namwachia yeye! Yangu na yaliyojiri Bungeni.. Najua jinsi ya kuyahandle. Yawezekana yalishamalizwa kabla ya Ibada yake LEO.”

About this writer:

Irari Ngugi

Lover of life, lover of big boobs and certified celebrity squasher. Catch me if you can on facebook as Irari Ngugi