Mchungaji Shillah Afungukia Swala la Rose Muhando

Mtumishi wa Mungu mchungaji Shillah amefunguka na kuongelea kile kinachoendelea kuongelewa katika mitandao ya kijamii kuhusu hali ya rose muhando ambae ni msanii wa injini nchini Tanzania ila kwa sasa yuko nchini Kenya .

Mwanadada huyo ambae aliripotiwa kuwa yu mgonjwa mautiuti na hata kabla ya hapo ailiwahi kusambaa video ikimuonyesha yuko kwa mchungaji akitolewa mapepo.

download latest music    

Mchungaji anasema kuwa watu wamekuwa wakimsema vibaya mchugaji aliyekuwa akimuombea rose muhando kwa madai kuwa hakufanya vizuri kwa sababu msanii mkubwa kama yule aliitaji usiri wa maombezi.

Mchungaji shillah anapinga hilo na kusema kuwa , watu wemgi wakubwa na maarufu wamekuwa wakiombewa  wanaonekana kwenye tv hata dunia nzima inakuwaje ishindikane kwa Rose Muhando.

Mchungaji anasema kuwa ni kweli kilichomkuta rose muhando ni pepo na wala sio vinginevyo.

Nilipofanya uchunguzi wangu wa kiroho niligundua kwamba , rose muhando kilichomkuta ni mapepo kweli sio uongo wala kiki na pia mimi nina mtetea mchungaji kwa sababu mimi ninapomtabiria mtu nikamrekodi kwanini akitokea staa nisikirushe? watu kama kina prophert joshua wanawatabiria maraisi na wanawaonyesha kwanini asiwe yeye , ile sio kiki.

About this writer:

Expedicto Lilian

#Godseeker, I am what i ought to be and always i will be, but am not what i used to be.