Birthday ya Lulu Kufanyika Muhimbili
Ikiwa leo ni siku ya kumbukumbu ya kuzaliwa ya msanii Lulu Michael ambae kwa upande wake hatoweza kuifurahia sana kutokana na mazingira anayoyapitia kwa sasa ya kutumikia kifungo chake cha miaka miwili gerezani na kwamba hawezi kuungana na watu anaowapenda.
Hata hivyo familia yake kwa kushirikiana na watu wake wa karibu na baadhi ya mashabiki wameamua kufanya sherehe hiyo kwa kwenda katika hospitali ya taifa ya muhmbili na kusherekea sikukuu hiyo na wagonjwa waliopoa hospitalini hapo.
Wakionekana katika mazingira ya hospitali upand wa wagonjwa wenye vichwa vikubwa , wawakilishi wa lulu watatoa zawadi na misaada kidogo kwa wagonjwa hao kama kumshukuru Mungu kuendelea kumlinda lulu huko alipo na kumuombea ili aweze kuwa na afya njema tena.
Wasanii mbalimbali na watu wake wa karibu wameweza pia kukumbuka siku hii kwa kuweka pichazake katiia mitandao ya kijamii akiwepo Wema Sepetu pamoja na mpenzi wake Majizo.