Barnaba Amkabidhi Mh Kingwangala Album ya Gold Wodini MOI.
Msanii wa muziki wa bongo fleva nchini, Barnaba classic amekwenda kumtembelea Waziri wa Maliasili na Utalii Mh Hamis kigwangala hospitalini MOI ambako alilaza tangu August 4 mwaka huu ambako alikuwa akipatiwa matibabu ya mkono uliovunjika kwa ajali aliyoipata alipokuwa kazini.
Ukiacaha na kwenda kumjulia hali, lakini pia Barnaba ahakusita kumkabithi waziri huyo album yake mpya ya Gold ambayo imetoka hivi karibuni na imekuwa ikipatikana katika maduka ya mitandaoni .
Hata hivyo mh Kigwangala amemshukuru sana Barnaba na kumwambia kuwa alipata mwaliko wake wa uzinduzi wa album hiyo lakini hakuweza kuhudhuria kutokana na hali yake aliyokuwa nayo lakini anampongeza sana kwa hatua aliyoweza kuifikia na anamuombea afanikiwe zaidi.
Nilipata mwaliko wako lakini sikuweza kuja kutokana na ajali,lakini ninaendelea vizuri na ninashukuru kwa kufika na kuja kuniona.natambua wasanii pia ni nguzo katika kukuza utalii wetu hasa wanapotmia mashairi na ndio maana mwezi septemba tuna tamasha la urithi festival ambalo pia wasanii wamepewa nafasi ya pekee.
Kwa upande wa Barnaba pia amemshukuru sana dk hamis kwa kupokea album hiyo lakini pia amempa pole kwa ajali .