Wasanii Tanzania Watoka Kapa Tuzo za AFRIMMA.
Usiku wa kuamkia october 8 ilikuwa moja ya siku muhimu kutokana na ugawji wa tuzo za AFRIMMA nchi Marekani ambapo kwa upande wa waliokuwa wakiwania tuzo pia wasanii kutoka Tanzania walikuwepo baadhi yao.
Hata hivyo mwaka huu umekuwa tofauti kwa wasanii wa Tanzania kutokana na kwamba wale wote waliowekwa katika kategoria mbalimbali hawakuweza kufanikiwa kuchukua tuzo hizo huku wasanii kutoka Uganda na Kenya wakiinuka kidedea katika tuzo hizo.
Wasanii kama Nandy, Alikiba, Ommy Dimpoz, Vannesa, Diamond Platnumz na pia Navy Kenzo walikuwa aktika kategorai mbalimbali,hata hivyo wasanii kutoka nchi za jirani kama Khaligarph Jones, na Eddy Kenzo waliweza kuibuka kidedea.