Wema Kula Sahani Moja na Omotola.
Mwanadada kutoka Tanzania, anaejulikana kama Tanzania Sweetheart Wema sepetu amefunguka na kusema kuwa bado ana matamanio makubwa sana ya kufanya kazi ya sanaa na wasanii wakubwa kutoka nje ya nchi hasa Omotola ajalade.
Akiongea na waandishi wa habari Wema alisikika akisema ” Natamani sana kufanya kazi na Omotola kutoka Nigeria na Inshalah ipo siku itakuwa kheri.”
Hata hivy wema naweza kujivunia mafanikio yake makubwa hasa baada ya kukamilisha kufanya kazi na msanii Van Vicker ambae wameweza kuzindua filamu yao hivi karibuni, hata hivyo wema aliwahi kuwa na historia ya kumleta mwanadada huyo nchini Tanzania.