Ndanda Fc wamshukuru harmonize kwa msaada aliotoa.
Msanii wa muziki Harmonize amewatoa kimasomaso wachezaji wa timu ya Ndanda fc baada ya kukwama katika hotel moja mjini singida walipokwenda kucheza mpira na timu ya Singida United na kufungwa goli 3-1 wiki iliyopita.
Hata hivyo wachezaji hao walikwamba hotelini hapo baada ya kuyumba kiuchumi lakini msanii huyo ambae ana mapenzi ya kweli na timu yake kutokea nyumbani Mtwara aliamua kujipiga na kutoa kiasi cha shilingi milioni tatu na laki tano kwa ajili ya kuwakwamua wachezaji na viongozi wao .
Wakitoa salamu zao za shukrani Timu hiyo ilimshukuru sana Harmonize lakini pia bila kuusahau uongozi wa msanii huyo amba ni Babu Tale na Diamond platinumz.