Rich Mavoko Afungukia Mahusiano Yake na Lulu Diva na Mipango Ya Ndoa

Msanii wa muziki wa Bongo fleva Richard Martin maarufu kwa Jina la usanii kama ‘Rich Mavoko’ amefunguka na kuweka wazi kuhusiana na tetesi za Mahusiano Yake na Lulu Diva.

Kunekuwa na tetesi za muda mrefu kuwa Rich Mavoko na Msanii mwenzake Lulu Diva wapo Kwenye Mahusiano ingawa wamekuwa wakikataa mara kwa mara lakini bado tetesi hizo zimekuwa zikiwaandama.

download latest music    

Kwenye mahojiano aliyofanya na Global Publishers, Rich Mavoko amefunguka na kuweka wazi kuwa hana uhusiano na Lulu Diva zaidi ya kikazi na kirafiki:

Hivi unajua sijawahi kusema au kukiri sehemu nina uhusiano na Lulu Diva! Nafikiri hayo ni mambo ya kazi na yameshapita”.

Lakini pia Mavoko amefungukia mipango ya kufunga ndoa hapo baadae na tofauti na wasanii wengi yeye anaamini kufunga ndoa hakuwezi kuharibu Taratibu za mtu kimuziki:

Sijaoa bado ila nina watoto wawili, lakini kuoa ni jambo la kheri sana wanaosema wakioa watashuka kimuziki kwa hiyo wataoa lini sasa, uzeeni? Kwangu mimi muda ukifika nitafanya hivyo“.

 

 

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.