Alichoandika Gerson msigwa kuhusu Ruge
Mkurugebzi wa mawasiliano ya Ikulu bwana Gerson Msigwa amekuwa moja ya viongozi wa serikali walioguswa sana na ugonjwa unaomkabili sasa hivi boai na mkurugenzi wa uzalishaji wa vipindi bwana Ruge mutahaba ambae amekuwa mgonjwa sasa kwa muda mrefu.
Ruge ambae anasemwa kuwepo Afrika ya Kusini kwa matibabu na mapumziko ya muda mrefu amekuwa akitolewa dua na maombi ya watu wengi tangu kutangazwa kuumwa kwake huku kila mtu akimlilia kutoka na kuwa amegusa maisha na mafanikio ya watu wnegi sana.
Gerson anasema kuwa kama ambavyo Ruge amekuwa mstari wa mbele kupIgania maisha ya wengine basi sasa anamuombea kwa Mungu li aweze kupigania maisha yake kwa sasa, huku akisistiza kuwa ni jukumu la kila mtanzania kumuombea.