Esther Kiama Atamani Nafasi Ya Jokate

Muigizaji wa Bongo movie Ester Kiama amefunguka na kuweka wazi kuwa ametokea sana kumtamania mrembo Jokate Mwegelo ambaye kwa sasa ni Mkuu wa Wilaya ya Kisarawe.

Kwenye mahojiano aliyofanya na Global Publishers, Ester alidai kuwa, kwa sasa Jokate amekuwa ‘role model’ wake na anaamini siku moja atakuwa kama yeye.

download latest music    

Unajua nimejikuta natamani kuwamkuu wa wilaya flani hivi ingawa najua siyo mchezo kama watu wanavyofikiria. Kiukweli Jokate ndiyo amenifanya nitamani hivyo, navutiwa na utendaji kazi wake lakini pia anavyonyuka zile suti. Na mimi nimeshaanza kumuiga katika uvaaji”.

Miezi michache iliyopita Mrembo Jokate Mwegelo aliteuliwa na Raisi Magufuli na kuwa mkuu wa Wilaya ya Kisarawe na mara moja mrembo huyo ameonekana kufanya vizuri sana katika nafasi yake na kuwatumikia vyema wananchi.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.