Abdu Kiba- Ninaweza Kufanya Kolabo na WCB Lakini Inategemea na Wimbo

Msanii wa Bongo fleva Abdul Kiba ambaye pia ni mdogo wa staa wa Bongo fleva Ali Kiba amefunguka na kudai kuwa yupo tayari kufanya Kolabo na mahsimu wao wakubwa WCB.

Sio siri kuwa Diamond na Ali Kiba hawapikiki chungu kimoja pamoja na kwamba wameshasema hawana bifu lolote lakini ni wazi kuwa Kumekuwa na tensions fulani baina ya makundi hayo mawili.

download latest music    

Lakini Abdu Kiba ameibuka na kudai kuwa kama ikitokea kuwa kuna wimbo ambao utakuwa na uhitaji wa msaniii kutoka WCB ndio ukae sawa hataona shida kumtafuta ili wafanye kazi.

Abdu Kiba amefunguka hayo Kwenye mahojiano na EFM Radio Lakini amejitetea Kuwa Mpaka sasa hajapata wimbo unaohitaji sauti kutoka kwa msanii yeyote wa WCB:

Kufanya kolabo na msanii yeyote kutoka WCB inategemeana na muziki gani ambao nimeimba, naamini kila muziki una sura ambayo inaonyesha ni nani unaweza kuimba naye, ikitokea kuna muziki ambao naona kuna haja ya msanii kutoka WCB nitafanya naye na kama sina tutabaki hivi hivi WCB na Team Kiba”.

 

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.